HABARI MPYA
blink
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Development stories. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Development stories. Onyesha machapisho yote
02:51
JE UNATAFUTA KAZI? HII NI NJIA BORA YA KUPATA AJIRA
Written By Unknown on Jumanne, 17 Novemba 2015 | 02:51
Ukosefu wa
ajira ni changamoto kubwa duniani kote. Hili linasikitisha kwa kuwa kazi ni
chanzo cha heshima binafsi, amani na utulivu.Tanzania, miongoni mwa nchi
za dunia ya tatu, imechukua hatua muhimu katika kuendeleza sekta yake ya ajira,
japo bado inakabiliwa na changamoto kubwa katika hilo. Asilimia kubwa ya
watanzania wenye uwezo wa kufanya kazi, aidha hawana ajira au ajira walizonazo
haziendani na uwezo wao.
Kutokana
na ushindani mkubwa katika soko la ajira na ongezeko kubwa la vijana wanaoingia
kwenye soko la ajira (800,000 hadi 1,000,000 kwa mwaka), sekta rasmi imekosa
mafanikio katika kuzalisha fursa za ajira, hasa mijini. Matokeo yake ni;
kiwango cha umasikini kimeongezeka.
Sababu kuu
zinazochangia fursa duni za ajira ni pamoja na:
· Kutokuwa
na usawa kati ya supply ya wafanyakazi na mahitaji. Ukweli ni kwamba, supply ya
wafanyakazi ni kubwa kuliko demand ya wafanyakazi katika soko la ajira. Kila
mwaka tunashuhudia ongezeko la vijana wanaomaliza masomo yao ambao wanaingia
mtaani kuongeza idadi ya watafutao kazi.
· Vijana
kukimbilia kutafuta kazi mijini. Asilimia kubwa ya vijana wakimaliza elimu yao,
hufikiria kwenda mijini kutafuta ajira, na wengi wao huwa na mawazo ya kufanya
kazi ‘za ofisini’. Hili linasababisha shinikizo na ushindani mkubwa wa fursa za
ajira. Laiti kama vijana wengi wangeamua kujikita katika sekta ya kilimo cha
kisasa au sekta nyingine tofauti tofauti kwa kutumia elimu yao, ongezeko la
watafutao kazi mjini lingepungua kwa kiasi kikubwa.
· Elimu
duni. Hili linajumuisha kutokujua kusoma na kuandika na ukosefu wa mafunzo
sahihi yanayomuandaa mtu kuingia katika soko la ajira. Hakuna mwajiri anayeweza
kuajiri mtu asiye na stadi muhimu za kitaaluma zinazohitajika katika kazi.
Inaaminika kuwa, zaidi ya 61% ya wahitimu wanakuwa hawako tayari kiushindani
katika soko la ajira.
Kutokana
na mwangaza huo wa hali halisi ya ajira nchini Tanzania mradi wa #RecruitMe umejipanga
kusaidia kila mwenye uwezo wa kufanya kazi, vijana na wazee ili waweze kupata
ajira wanazotaka. Tunafahamu kwamba ukosefu wa kazi ni jambo linalotatiza wengi
na wengi kuhisi kuwa wamenyimwa haki yao kama binadamu ndani ya jamii
wanayoishi.
Kwa
hiyo, #RecruitMe kwa makusudi mazima imeamua
kujitolea kuweka jukwaa ambalo kila mtu anaweza kulitumia anapotafuta ajira
sahihi na kupitia jukwaa hilo, mtu anaweza kugundua fursa mpya zilizopo katika
soko la ajira. Zaidi ya hayo, waajiri wanaweza kunufaika sana kutokana na
jukwaa hili, kwa kuwa linatoa fursa kwao pia kutafuta wafanyakazi
wanaowahitaji.
Lengo kuu
la mradi huu si kuwapa watu ajira yeyote tu, la hasha, bali ni kuwapatia watu
ajira zenye hadhi, heshima na kufanya ndoto za mtu kuwa kweli. #RecruitMe itakupatia
ajira inayokubalika kisheria, yenye mapato yanayoendana na kiwango cha kazi na
ujuzi wako. Tunakuthibitishia ajira itakayojali haki zako kama mwanadamu na
mfanyakazi, ikiwa ni pamoja na kujali maslahi yako.
Ili kupata
huduma zetu, tafadhali tembelea tovuti yetu http://goo.gl/zPLquy ambapo
utakuwa na uwezo wa kuona fursa za ajira mbalimbali, pamoja na kujenga profile
yako mwenyewe. Huna haja tena ya kutokwa na jasho kutembea kutoka ofisi moja
hadi nyingine tu na kuishia kunyimwa nafasi. Pumzika, na tembelea tovuti yetu.
Tunaweza kukusaidia kupata kazi uitakayo.
Labels:
Development stories
09:07
Imeelezwa kuwa mfumo dume ni moja ya changamoto
zinazokwamisha wananwake nchini Tanzania katika harakati za kushiriki uongozi
wa kijamii na uchumi.
MFUMO DUME WAKWAZA WANAWAKE TANZANIA
Written By Unknown on Alhamisi, 2 Oktoba 2014 | 09:07
Hayo yamebainishwa na afisa kutoka shirika la umoja wa
mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO, Bi. Rose Mwalimu katika
mahojiano maalumu.
Bi. Rose amebainisha kuwa wanawake wananyimwa fursa kutokana
na mfumo dume jambo ambalo linatia shaka kama usawa wa hamsini kwa hamsini
utapatikana ifikapo 2015 katika uwakilishi wa vyombo vya maamuzi.
Aidha Bi. Rose amebainisha kuwa licha ya jamii kutegemea
vyombo vya habari katika kubadili tabia kwa njia ya habari, bado waandishi wa
habari Tanzania havijatoa mchango wake kuondoa mfumo dume na unyanyasaji wa
kijinsia
Akielezea juu ya weledi wa waandishi wa habari Tanzania Bi
Rose mwalimu ambaye pia kitaaluma ni veteran katika taaluma ya habari,
amewatahadharisha waandishi wa habari kuwa makini na waepuke kuandika habari
zenye kuchochea migogoro.
Shirika la UNESCO linaendesha mafunzo kwa waandishi wa
habari kutoka katika Radio jamii nchini ili kuwajengea uwezo wa kuandika habari
na kuandaa vipindi kwa kuzingatia masuala ya jinsi na jinsia.
Zaidi ya Radio Jamii 11 zimepata udhamini wa mafunzo na
kujengewa uwezo na UNESCO ambayo yamefanyika kati ya September 22 na October
mosi ambayo yamefanyika mkoani Kigoma pamoja na Mwanza.
Labels:
Development stories
09:42
WAHANGA WA MVUA 2013 WATELEKEZWA KIGOMA
Written By Unknown on Jumapili, 14 Septemba 2014 | 09:42
Na. Emanuel Senny, Kigoma.
WAHANGA 100 wa mafuliko yaliyotokea mwaka 2013 maeneo ya katosho, kata ya Kibirizi katika manispaa ya Kigoma Ujiji wameachwa bila msaada wowote huku wakiishi maisha ya kutangatanga sambamba na kutotakiwa kujenga upya kutokana na eneo hilo kutengwa ili kupisha ujenzi wa bandari ya nchi kavu.
Akifafanua hilo Mjane Bahati Luseba alisema yeye ni miongoni mwa wahanga ambapo alipoteza nyumba yake na anaoishi kwa kutangatanga kutafuta mahali pa kuishi hali inayowalazimu watoto wake watano wakiwemo wawili wa kike walale katika nyumba isiyosalama huku akisubiri fedha za fidia ambazo hajui atapewa lini.
Alisema aliishi hapo zaidi ya miaka 40 ndipo Desemba ,2013 walipokutwa na mafuriko, ambayo yalibomoa nyumba yake na kumlazimu alale nje zaidi ya miezi kumi akisubiri hatma ya malipo ya fidia kutoka serikalini ili aondokane na adha ya kutangatanga .
Baada ya nyumba yangu kuharibika, mganga wa zahanati ya jibulenu alinipa chumba kwa muda katika zahanati yake , na kwasasa nimesaidiwa na mwalimu Gombea baada ya kutoka kutoka katika Zahanati kwani ni mahari pa wagonjwa tu alisema Luseba.
Aliongeza kuwa taarifa zilizotoka Halmashauri kuwa kuna nyumba alitaftiwa kwaajiri ya makazi sio kweli pia mahema ambayo inasemekana walipewa baadhi ya wahanga hakuziona kwahiyo taarifa sio za kweli kwani yeye bado anatangatanga.
Dkt. wa Zahanati ya Jibulenu Abu Rashid alikiri kumhifadhi katika chumba kimoja katika zahanati kutokana na mvua zilizokuwa zikiendelea.
Aidha Kagu Jumanne ambaye ni mmoja wa wahanga wa mafuriko alisema kuwa baada ya tukio viongozi walienda eneo husika na kuahidi kutoa msaada kwa waathirika wote ila mpaka sasa hakuna walichopewa na wanaendelea kuhifadhiwa kwa majirani.
Akijibia malamiko hayo Diwani wa kata husika Rashid Yunus ambaye pia ni Kaimu Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji alisema changamoto ya kushindwa kuwasaidia wahanga wa mafuriko inatokana na idadai kubwa ya walengwa na walitoa tulubai 52 kwa kaya 9 sambamba na kuyafungia mabati ili kuepusha lawama kwa umma kutokana na hali duni za wahanga hao.
Hata hivyo Yunus alisema kuwa manispaa, ilitoa mabati chakavu 70, ili wapewe wananchi wenye maisha duni , lakini kutokana na ukubwa wa familia hizo wameamua kuyafungia katika ofisi ya serikali ya mtaa wa kahabwa katosho wakisubiri mchakato wa kufidiwa kwa wahanga hao ambao eneo lao limeteuliwa kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Bandari kavu.
![]() |
| Bi. Bahati Luseba akiwa na wanawe katika eneo ilipokuwa nyumba yake |
WAHANGA 100 wa mafuliko yaliyotokea mwaka 2013 maeneo ya katosho, kata ya Kibirizi katika manispaa ya Kigoma Ujiji wameachwa bila msaada wowote huku wakiishi maisha ya kutangatanga sambamba na kutotakiwa kujenga upya kutokana na eneo hilo kutengwa ili kupisha ujenzi wa bandari ya nchi kavu.
Akifafanua hilo Mjane Bahati Luseba alisema yeye ni miongoni mwa wahanga ambapo alipoteza nyumba yake na anaoishi kwa kutangatanga kutafuta mahali pa kuishi hali inayowalazimu watoto wake watano wakiwemo wawili wa kike walale katika nyumba isiyosalama huku akisubiri fedha za fidia ambazo hajui atapewa lini.
Alisema aliishi hapo zaidi ya miaka 40 ndipo Desemba ,2013 walipokutwa na mafuriko, ambayo yalibomoa nyumba yake na kumlazimu alale nje zaidi ya miezi kumi akisubiri hatma ya malipo ya fidia kutoka serikalini ili aondokane na adha ya kutangatanga .
Baada ya nyumba yangu kuharibika, mganga wa zahanati ya jibulenu alinipa chumba kwa muda katika zahanati yake , na kwasasa nimesaidiwa na mwalimu Gombea baada ya kutoka kutoka katika Zahanati kwani ni mahari pa wagonjwa tu alisema Luseba.
![]() |
| Mabaki ya nyumba ziliezuliwa na Kimbunga wakati mvua kali |
Dkt. wa Zahanati ya Jibulenu Abu Rashid alikiri kumhifadhi katika chumba kimoja katika zahanati kutokana na mvua zilizokuwa zikiendelea.
Nilishindwa kuendelea kumhuhifadhi kutokana na sheria,kanuni na taratibu za kikazi kuwa, zahanati si makazi rasmi kwa asiye mgonjwa aliongeza Rashidi.
Aidha Kagu Jumanne ambaye ni mmoja wa wahanga wa mafuriko alisema kuwa baada ya tukio viongozi walienda eneo husika na kuahidi kutoa msaada kwa waathirika wote ila mpaka sasa hakuna walichopewa na wanaendelea kuhifadhiwa kwa majirani.
Akijibia malamiko hayo Diwani wa kata husika Rashid Yunus ambaye pia ni Kaimu Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji alisema changamoto ya kushindwa kuwasaidia wahanga wa mafuriko inatokana na idadai kubwa ya walengwa na walitoa tulubai 52 kwa kaya 9 sambamba na kuyafungia mabati ili kuepusha lawama kwa umma kutokana na hali duni za wahanga hao.
Hata hivyo Yunus alisema kuwa manispaa, ilitoa mabati chakavu 70, ili wapewe wananchi wenye maisha duni , lakini kutokana na ukubwa wa familia hizo wameamua kuyafungia katika ofisi ya serikali ya mtaa wa kahabwa katosho wakisubiri mchakato wa kufidiwa kwa wahanga hao ambao eneo lao limeteuliwa kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Bandari kavu.
Labels:
Development stories
03:41
MAONESHO YA BIASHARA SIDO KIGOMA 2014 YAFANA
Written By Unknown on Jumanne, 2 Septemba 2014 | 03:41
![]() |
| Bw. McDonald Maganga, Meneja wa SIDO Kigoma |
Maonesho ya bidhaa zinazozalishwa na viwanda vidogovidogo
kanda ya kati yamemalizika kwa mafanikio makubwa mjini Kigoma nchini Tanzania huku yakiacha
changamoto kadhaa za mitaji na masoko ya bidhaa husika.
Washiriki wa maonesho hayo kutoka mikoa ya Dodoma, Singida,
Tabora na mwenyeji Kigoma wamekiri kuwepo kwa matatizo ya mitaji pamoja na
ukosefu wa soko la uhakika ndani na nje ya nchi, jambo linalodhoofisha wamiliki
wa viwanda na wajasiriamali.
![]() |
| Sehemu ya Mabanda yaliyotumika katika maonesho ya biashara maarufu kama maonesho ya SIDO Kigoma |
Wakiongea na mtandao huu katika kilele cha maonesho hayo wameomba serikali na taaisisi zake kuwawezesha
wajasiliamali kupata mitaji kwa njia ya mikopo yenye riba nafuu pamoja fursa za
masoko.
Mmoja wa washiriki wa maonesho hayo Bi. Cotrida Kokupima
kutoka wilayani Kasulu Mkoani Kigoma, amesema licha ya serikali kuwa na sera nzuri za kusaidia wajasiriamali bado
taasisi za fedha hasa Benki hazijatoa unafuu kwao.
Naye Bw.Hamis Rudonongo kutoka Dodoma amesema watumishi wa
umma katika kada ya chini, wanakiuka maadili ya utumishi wao kwa kuwanyima
huduma wajasiriamali wadogo.
Kwa upande wake meneja wa shirika la
maendeleo ya viwanda vidogo SIDO mkoani Kigoma Bw. McDonald Magnaga ambaye ndiye alikuwa
mwenyeji wa maonesho hayo amesema licha ya changamoto zinazotajwa na wadau,
maonesho hayo ya mwaka yamekuwa ufunguo wa fursa za masoko
Licha ya kukiri kuwepo kwa tatizo la soko la nje ya Tanzania,
McDonald amebainisha kuwa SIDO inao mfuko maalumu kwa kuwakopesha Mitaji wajasiriamali
wanaotimiza vigezo.
Bw. McDonald Maganga amebainisha kuwa Shirika hilo la viwanda
vidogo linazo fursa za mikopo ambapo waasiriamali hukopeshwa kati ya sh.
milioni mbili hadi sita.
Zaidi ya wajasiriamali 270 kutoka mikoa ya kanda ya kati pamoja
na nchini Kenya wameshiriki maonesho hayo.
Kwa mujibu wa taarifa za SIDO kiasi cha zaidi ya shilingi
milioni mia mbili kimekopeshwa kwa wajasiriamali wadogowadogo katika kipindi
cha mwaka 2013/2014
Labels:
Development stories
09:22
MAONESHO YA WANASAYANSI CHIPUKIZI (YOUNG SCIENTISTS) TANZANIA YAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM
Written By Unknown on Alhamisi, 21 Agosti 2014 | 09:22
![]() |
| Sanamu ya Ndege iliyoungwa na mmoja wa wanasayansi chipukizi wa Tanzania |
Na. Mwandishi wetu
Dar es Salaam
Maonesho pamoja na sherehe ya kuwatunukia zawadi
washindi wa wanasayansi chipukizi au Young Scientists Tanzania (YST)
yalifanyika tarehe 13 hadi 14 mwezi Agosti
katika ukumbi wa Aghakhan Diamond Jublee.
Maonesho haya walifadhiliwa na British Gas Tanzania pamoja na Irish Aid kwa matarajio kuwa vijana hawa wakiendelezwa tatizo la afrika kukosa wana sanyansi litakwisha
Mgeni rasmi wa maonesho hayo alikua Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dr. Mohammed Gharib Bilal akifuatana na Balozi
wa Ireland nchini Tanzania Finneoula Gilsenan pamoja na Waziri Prof. Makame M.
Mbarawa ambao pia walihudhuria maonesho hayo
![]() |
| Makamu wa Rais Dr. Gharib Bilal akisalimiana na meneja wa kampuni ya British Gas Bw. Adam Prince wakati wa Maonyesho hayo |
Wanafunzi 200
na walimu kutoka mikoa mbalimbali Tanzania walikusanyika jijini Dar es Salaam
kuonyesha miradi yao ya utafiti mwaka huu.
Ongezeko la msaada unaotolewa na BG(British Gas) Tanzania na Ireland Aid (Shirika
la msaada la Ireland),kumewezesha maonyesho ya wanasayansi chipukizi kuwafikia wanafunzi vijana kwa wingi zaidi ndani ya mwaka huu 2014.
Maonyesho ya( YST ) 2014 ni muendelezo wa mafanikio
yaliyofikiwa miaka ya nyuma kutoka shule 4 mwaka 2011 hadi kufikia shule 100 mwaka huu.
![]() |
| Robn Damas na Michael Laurent wanafunzi kutoka Ilboru sekondari wakifurahia tuzo |
Programu ya YST ilitokana na
jitihada za Ireland ambayo ilitumia mfumo wa maendeleo ya elimu kupitia (CDPC)
Combat Diseases of Poverty Consortium. (Kundi
la kupambana na maradhi yanayotokana na umaskini.
Wanafunzi watakaoshinda watawezesha shule zao kukua
kisayansi na maendeleo. Zawadi zilizomo ni laptops, fedha, scholarships, pamoja
na vitabu kwa maktaba za shule. Washindi wa jumla wa YST 2014 wataalikwa kuhudhuria maonyesho
ya BT Young Scientists na Teknolojia yatakayofanyika nchini Ireland mnamo Januari 2015.
Kila mwaka maonyesho YST yanalenga kuongeza mafanikio katika jitihada za kuinua kiwango cha elimu ya sayansi katika
shule za sekondari Tanzania .
Maonyesho
yanaelezea miradi kutoka makundi mbalimbali ya sayansi,
kibaiolojia na ikolojia; fizikia na kemia; masomo ya kijamii na kitabia; na
teknolojia.
Young Scientists Tanzania inatoa wito kwa shule zote
nchini kujipatia fursa ya kukua kisayansi na kubadilisha mfumo wa kujifunza masomo
ya Sayansi kwa kupitia mashindano hayo. Mashinda hayo hufanyika kila mwaka
jijini Dar es Salaam na huhusisha zaidi ya shule 100.
Labels:
Development stories

.jpg)
.jpg)





